Kiungo wa kati wa Manchester United Paul Pogba amesema hababaishwi na semi za kila mara kutoka kwa wachambuzi wa soka Uingereza na kwamba amezoea matamshi yao ya kila mara kumhusu.
Mchezaji huyo wa Ufaransa ambaye alijiunga na klabu hiyo ya Uingereza akitokea klabu ya Italia Juventus mwaka 2016, alicheza mechi yake ya mwisho kabla ya kupata jeraha mnamo disemba mwaka jana dhidi ya Newcastle mechi ambayo walisajili ushindi wa magoli 4-1.
Miongoni mwa watu ambao wamekuwa wakimsema kiungo huyo ni mchezaji wa kitambo wa klabu ya Liverpool Graeme Souness ambaye alimtaja kiungo huyo kama mtu mnafiki inapowadia wakati wa kucheza.
Aidha mchezaji huyo alikwa anatarajiwa kushirikishwa katika mechi za hivi karibuni za klabu ya Manchester United, japo kutokana na virusi vya Corona ligi hiyo ilisitishwa kwa muda.
Alikuwa anauguza jeraha la kinena baada ya kufanyiwa upasuaji na madaktari.
MHARIRI: DAVIS OJIAMBO
