logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Achana na sideshows hazileti shangwe.' Arrow bwoy amwambia Nadia Mukami

'Achana na sideshows hazileti shangwe.' Arrow bwoy amwambia Nadia Mukami

image
na

Habari02 October 2020 - 06:33
mukami
Mwanamuziki Arrow bwoy amezungumza kwa mara ya kwanza akimshauri msanii mwenzake Nadia Mukami. Arrow Bwoy alimwambia kuwa aachane na Sideshows ambazo hazimsaidii katika sanaa ya muziki.

Kwa muda saa, Nadia amekuwa akitoa vibao akiwashirikisha wasanii wenzake mbalimbali, lakini kwa maoni ya Arrow Bwoy azingatie sanaa ya usanii wake.

Uvumi umekuwa ukienea hapa na pale kuwa wawili hao ni wapenzi ambapo walikataa. Hii ni baada ya kutoa kibao cha 'radio love' pamoja baadae wawili hao walikiri kuwa uvumi huo ulikuwa wa ukweli ilhali mapenzi yao hayakutoboa.

“He’s an amazing friend. We tried dating but it didn’t work." Nadia Alisema.

Nadia alizidi na mazungumzo na kusema kuwa Arrow Bwoy aliendelea na maisha siku mbili tu baada ya kuachana.

Msanii Arrow amekuwa akikwepa drama hizo, lakini amezungumza akimshauri azingatie malengo yake.

"I’ll give some advice to Nadia Mukami. She is one of the vibrant female artistes in East Africa. She has so much potential in raising our Kenyan  flag high. However, she can only reach these heights once she channels all her energy into her craft." Alisema Arrow Bwoy.

Alizidi na kusema kuwa yeye ni shabiki wa Nadia na anapaswa kutilia maanani usanii wake,

“Aachane na hizo sideshows, hazileti shangwe yaani. Because the Nadia I know is the one I did a collabo with and I love the fact that she is a go-getter. Piga tu kazi. I’m your fan." Arrow Bwoy Alizungumza.

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved