logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Liverpool yasingizia klabu ya Athletico Madrid kuwa ilichangia pakubwa kuenea kwa Corona katika mjini humo

Liverpool yasingizia klabu ya Athletico Madrid kuwa ilichangia pakubwa kuenea kwa Corona katika mjini humo

image
na

Habari02 October 2020 - 06:33
NA NICKSON TOSI

Katika tukio la kustaajabisha malimwengu ya Soka ni kuwa mkuu wa mji wa Liverpool Steve Rotheram sasa amewataka wasimamizi wa dimba la ligi ya mabingwa kuanzisha uchunguzi kubaini iwapo Athletico Madrid ilichangia pakubwa kusambaa kwa virusi vya Corona ambavyo vimeathiri mji huo.

Mtanange wa makundi awamu ya 16 bora uliochezwa Machi 11 na ambao klabu hiyo ililazwa magoli 3-2 na kutolewa na kubanduliwa nje ya dimba hilo na kushuhudiwa na mashabiki takriban 52, 000, wale waliotoka Uhispania wakiwa 3,000.

Baada ya mchuani huo, taifa la Uhispania lilifunga shughuli zote za spoti kutokana na mkurupuko wa virusi hivyo ambavyo vilikuwa vimeanza kuathiri maelfu ya watu.

Mshauri wa utafiti katika serikali kuu ya Uingereza Angela McLean amesema matamshi ya kiongozi huyo ni ya kustaajabisha sana na kueleza kuwa ameshangazwa na madai hayo.

MHARIRI: DAVIS OJIAMBO


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved