logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hatima ya Russia kushiriki katika mashindano ya olimpiki kubainika Novemba

Hatima ya Russia kushiriki katika mashindano ya olimpiki kubainika Novemba

image
na

Habari02 October 2020 - 09:04
skysports-russia-olympics-athletics_4946081
Hatima ya taifa la Urusi ama Russia ya kushiriki katika michezo ya Oilimpik itabainika kati ya Novema 2-5 mwaka huu.

Urusi ilikuwa imewasilisha kupinga hatua ya bodi ya World Anti-Doping Agencey WADA ya kuipiga marufuku ya miaka minne kutokana na hatua ya ongezeko la wanariadha wake kuendelea kutumia dawa za kusisimua misuli.

Kupitia ukurasa wa mtandao wa mahakama ya kusuluhisha mizozo ya michezo almaarufu kama Court of Arbitration for Sports CAS, Shirikisho la Riadha la Urusi limetangaza kupinga hatua hiyo.

 Baadhi ya marufuku ambayo yaliwekewa Urusi ni wanariadha wake kutoshiriki katika michezo yoyote ya Olimpiki ama Paralympic huku mashindano ya Olimpiki yakitarajiwa kufanyika mjini Tokyo iwapo virsui vya corona vitazuiwa.
Vile vile Urusi ilikuwa imepigwa marufuku ya kuandaa michezo huku wanariadha wa taifa hilo ambalo hawana makosa yoyote ya kutumia dawa za kusisimua misuli wakiruhusiwa kushiriki katika mashindano mengine.
Uchunguzi wa WADA ulibaini kuwa maabara nchini Moscow ilitoa taarifa za uongo kuhusiana na vipimo vya wanariadha wa taiafa hilo kati ya mwaka 2012-2015 .

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved