Auma ameelezea kusikitishwa na tukio hilo na kusema Malik anafanya hivyo kutokana na wivu baada ya Barack Obama kuwa rais wa Amerika.
Malik alikuwa ametundika cheti ghushi kilichokuwa kinaonyesha tarehe ya kuzaliwa kwa Barack Obama kilichoonyesha kuwa kiongozi huyo wa zamani wa Amerika alizaliwa Agosti mwaka 4,1961 katika hospitali kuu ya Coast General Mombasa, Jamhuri ya Kenya.
Wakenya katika mitandao ya kijamii almaarufu kama KOT, waligutushwa na kukejeli cheti hicho na kudai kuwa taifa la Kenya lilifahamika kama Jamhuri ya Kenya mwaka 1964 bali si 1961 kama ilivyokuwa imeandikwa kwa cheti hicho.
Wengine walibaini kuwa msajili aliyekuwa ametia saini katika cheti hicho hakuwa wa humu nchini bali kilikuwa kimeandikwa Australia.
Auma kama njia ya kumjibu vyema Malik, alisema amekuwa akiishi na machungu haswa baada ya Barack Obama kuwa rais wa taifa la Amerika.
Malik is consumed and driven by jealousy and bitterness towards President Obama “that you will go to any length to slander your younger brother’s name-literally.” Just because he has outshone you in every single aspect of his life. Seek relevance elsewhere big brother,”alisema Auma Obama
