logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jackpot! Kutana na Bilionea wa Tanzania Saniniu Laizer aliyepata mawe ya Tanzanite yenye thamani ya mabilioni

Jackpot! Kutana na Bilionea wa Tanzania Saniniu Laizer aliyepata mawe ya Tanzanite yenye thamani ya mabilioni

image
na

Habari02 October 2020 - 08:08
Mtanzania Saniniu Lazier ambaye ni mchimbaji madini mdogo amepata madini ya Tanzanite ambayo ya thamani ya bilioni 7.8.

Madini Hayo ambayo moja lina kilo 9.2 lina thamani ya bilioni 4.5 na la pili lina kilo 5.8 lenye thamani ya shilingi bilioni 3.3.

Aidha baada ya kupata madini hayo bwana Laizer aliyafikisha katika kituo cha utambuzi. Na hii leo serikali ya Tanzania imeyanunua madini hayo kwa thamani ya bilioni saba na milioni mia saba za kitanznaia.

Madini hayo yamekabidhiwa kwa serikali na bwana Lazier ambaye ni mkazi wa Simanjiro amepatiwa fedha zake huko Mkoani Arusha kaskazini kwa Tanzania.

Kupitia mtandao wa Twitter wizara ya madini ya Tanzania imemtambua mtanzania huyo kama bilionea.

Kwa mujibu wa wizara ya madini nchini humo maadini ya uzito huo hayajawahi kupatikana katika machimbo ya Tanzanite

Tanzanite ni madini yanayopataka na kuchimbwa nchini Tanzania pekee.

Mauzo ya madini hayo kwa mwaka 2019 duniani yalikua zaidi ya dola milioni 50 za kimarekani.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved