logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mtu yeyote atakaye panga 'paybill' ya mazishi yangu itakuwa ni kashfa-Akothee

Mtu yeyote atakaye panga 'paybill' ya mazishi yangu itakuwa ni kashfa-Akothee

image
na

Burudani01 October 2020 - 11:10
109532631_163034561946923_807964317432237429_n
Msanii Akothee amewaacha wengi midomo wazi hii ni baada ya kupeana maagizo ya jinsi atakavyo zikiwa akifariki, endapo mambo yatakuwa mabaya na kupumua pumzi yake ya mwisho.

Kupitia ujumbe aliounakili kwenye mitandao ya kijamii ya instagram Akothee aliweka wazi kuwa gharama ya hospitali italipwa na bima yake na kama haitatosha kulipa mali yake itauzwa ili gharama hiyo ilipwe.

Pia alinakili kuwa mtu yeyote asijaribu kutengeneza 'paybill' ya kulipa mazishi yake au mchango wa mazishi yake kwa maana amepanga hayo yote.

"Familia ni familia ata nikiwa kwenye kitanda changu cha kifo, dada yangu mkwe alizikwa kama sikuwa kwa maana nilikuwa napigana na maisha yangu katika hospitali ya Karen

Lakini nililipa kila kitu nilikuwa inahitajika nilinunua nguo na hata jeneza la mazishi, sina wazo lolote kwa nini nisiweze jilipia gharama yangu ya hospitali

Na hata kushughulikia wengine mimi ni nani mwanamke asiyejijali

Kama vile nilivyowaambia awali, nina bima ya hospitali nimekata bima kwa ajili ya mtoto wa dada yangu na mama yangu bima haingeweza kukata baba yangu kwa ajili ya umri wake

Niko sawa kulipa gharaa yake ya hospitali kutoka kwa mfuko wangu, kwa hivyo kama haya yote yamisha na nibaki bila pesa tafadhalini uzeni mali yangu niweze kuzikwa

Jeneza langu tayari limeshughulikiwa, cha mwisho pia nina bima ya mazishi mtu yeyote atakaye kuja na mpango wa paybill ili nizikwe itakuwa ni kashfa." Aliandika Akothee.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved