logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wakili John Khaminwa , 84 asema ni kifo tu kitakachomzuia kuendelea na sheria

Wakili John Khaminwa , 84 asema ni kifo tu kitakachomzuia kuendelea na sheria

image
na

Habari01 October 2020 - 10:23
kHAMINWA
Wakili mkongwe Dr John Khaminwa amekuwa jina tajika katika sheria nchini kwa muda mrefu na akiwa na umri wa miaka 84 sasa ungemtaraji kuwa nyumbani akipumzika lakini anasema kamwe hakomi kuendelea na shughuli zake za uanasheria  labda kifo tu ndicho kitakamzuia kuendelea na kazi yake .

Amekuwa mstari wa mbele kupigania haki na usawa humu nchini na pia ameyapitia mazito katika maisha yake .

“ Nampeza sana mke wake  alikuwa jaji mzuri sana’ ameliambia gazeti la The Star . Joyce Khaminwa  ,mke wake  wa miaka 48 aliaga dunia mwaka wa 2014 katika Nairobi Hospitali .alikuwa jaji wa mahakama kuu wakati huo .

“ Naam , tulikuwa na ndoa nzuri sana kwa miaka 48  .alikuwa mtu mzuri sana’ amesema Khaminwa huku huzi ikitanda wazi usoni mwake  .Huenda kfo kilimpokonya  ndoa  aliyoijenga kwa nguvu na hali zote .

Dr Khaminwa ana jingine pia la kumpa huzuzi anapozungumzia kifo cha mwnawe wa kwanza Albnert Khaminwa aliyeaga dunia mwaka wa 2017  akimtaja kama mmoja wa waliofuata nyayo zake kwa kuwa wakili  . Albert  alikuwa amefika kiwango chakuwa mshirika katika   kampuni yao ya uanasheria ya  Khaminwa & Khaminwa Advocates.

“ Alikuwa mtoto mwerevu sana’ wakili huyo anasema huku ikionekana wazi kwamba vifo vya wapendwa hao wake wawili vimeacha pengo kubwa sana katika maisha yake .

Anakaribia kugonga miaka 84  na ameshuhudia vitu vingi sana vingine vilivyomsadia na vingine havijamchangia chochote katika maisha yake  .Kinachomtoa mawazo ni kuendelea kufanya kazi yake ya uwakili kwa miaka 50 hadi sasa  .Kazi hiyo yake ndio inayomfanya kuamka kila siku na kutojawa na mawazo kuhusu vitu vingi vinavyofanyika katika  maisha yake .

“ kuwa wakili ni jambo la kipekee .napenda sana kusikiliza matatizo ya watu ,inaniondoewa mawao’ amesema

Khaminwa anapenda sana sheria na hayuko tayari kustaafu  anasema ni kifo pekee kitakachomzuia kuendelea  na kazi ya uwakili .

Dr Khaminwa amewaakilisha watu wenye majina tajika  wakati wa taaluma yake iliyodumu nsu ya karne  huku baadhi ya kesi zikimletea uhasama na  rais mstaafu Daniel Moi na hata akajipata amefungwa jela .

“ Nimewaakilisha Raila, Matiba, George Anyona  miongoni mwa wenine katika mapambanao dhidi ya utawala wa kiimla’ anasema Khaminwa . Hatua yake ya kumwakilisha  Stephen Mureithi,  aliyekuwa amehamishwa kama naibu mkuu wa idara ya ujasusi ni hatua ambayo ilimhamakisha sana rais Moi

Kesi nyingine tajika aliyoishughulikia ni  ilyohusisha utata wa kimila kati ya ukoo wa Umira Kager  kutoka  Alego dhidi ya  Wambui Otieno ambaye alitaka mwili wa mume wake  SM Otieno  kuzikwa nyumbani kwao  Ngong Matasia mwaka wa  1986. SM Otieno alikuwa wakili tajika enzi hizo na Dr Khaminwa alimwakilisha mjane  Wambui

Khaminwa alishinda  raundi ya kwanza wakati mahakama kuu ilipoagiza mjane kupewa mwili ili auzike Ngong lakini ukoo huo ukashinda kesi baada ya kukata rufaa na mwili ukapelekwa Alego ,Siaya

Ilikuwa mojawapo ya kesi zilizochukua muda mrefu –zaidi ya mwaka mmoja huku mwili wa SM Otieno ukisalia katika hifadhi ya maiti ya City

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved