logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Soma walichokuwa wanataka kufanya Tanasha Donna na Kevin Omwenga kabla ya kifo chake

Soma walichokuwa wanataka kufanya Tanasha Donna na Kevin Omwenga kabla ya kifo chake

image
na

Dakia-udaku01 October 2020 - 09:56
Mwendazake mwanabiashara Kevin Omwenga alifahamika sana kupitia kwenye mitandao ya kijamii na hata na watu tofauti kwenye tasnia ya usanii.

Omwenga aliuawa Jumamosi iliyopita baada ya kupigwa risasi kifuani mwake.

Washukiwa wakuu wa mauaji hayo Chris Obure na Robert Ouko wamo mikononi mwa polisi huku uchunguzi ukizidi kufanyika, kablla ya kifo chake Omwenga alikuwa amenunua gari mbili moja ikiwa ni ya aina ya Porsche Panamera inayo nunuliwa kwa millioni 14.

Meneja wake msanii na mtangazaji Tanasha Donna, Castro amesema kuwa mwendazake alikuwa anataka kufanya kazi na Tansha kabla ya kukumbana na mauti yake.

"Mungu pekee ndiye anajua natamani ungefuata njia ambayo ulikuwa umepanga na Tanasha Donna kuwa mmoja wa hudam ya jamii ya Tanasha

Labda ungekuwa hai sasa G wangu lakini Mungu anajua bora lala salama Kev almaarufu Rich Man."Meneja wa Tanasha Aliandika.

Kulingana na upasuaji Omwenga alipigwa risasi kwa makusudi na wala si bahati mbaya wala ajali kama vile alivyodai Ouko.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved