logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Haujanisikia nikilalamika,' DP Ruto aeleza kwanini urafiki wake na rais wa Uhuruto ulikwisha

'Haujanisikia nikilalamika,' DP Ruto aeleza kwanini urafiki wake na rais wa Uhuruto ulikwisha

image
na

Burudani01 October 2020 - 09:50
Huku akiwa katika mahojiano na runinga moja humu nchini naibu rais William Ruto alifungua roho yake kuhusu chama cha Jubilee na uhusiano wake na rais Uhuru Kenyatta.

Kama vile walivyodai kuwa hayupo serikalini Ruto alikuwa na haya ya kueleza kuhusu madai hayo na uhusiano baina yake na rais,

"Katika uongozi wetu wa muhula wa pili rais aliamua kufanya mambo kwa niia tofauti, na kwangu mimi nikachukua kiti cha nyuma ilikuwa Uhuruto wakati wa kwanza lakini katika uongozi wa pili watu wengine waliamua iwe Uhuru pekee

Ili tuweze kusema Uhuru ndiye kiongozi wa serikali, haujanisikia nikilalamika, hali yangu na rais imekubaliwa." Aliongea Ruto.

Huku akizungumzia utata ulio katika chama hicho Ruto alisema kuwa muda upo wa kusuluhisha matatizo hayo na iwapo suluhu haitapatikana ataweza kuruka nje.

"Matatizo ni ya viongozi kutatua. Hatuwezi kupotea, lakini ikishidikana kuna namna nyingi kwa siasa. Kwa mfano wakati mheshimiwa rais aliona kuna matatizo mengi aliunda chama cha TNA

Mimi pia wakati niliona chama cha ODM kimekuwa na udikteta, niliamua vingine. Lakini naamini bado hatujafika kuamua vingine."

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved