Kama vile walivyodai kuwa hayupo serikalini Ruto alikuwa na haya ya kueleza kuhusu madai hayo na uhusiano baina yake na rais,
"Katika uongozi wetu wa muhula wa pili rais aliamua kufanya mambo kwa niia tofauti, na kwangu mimi nikachukua kiti cha nyuma ilikuwa Uhuruto wakati wa kwanza lakini katika uongozi wa pili watu wengine waliamua iwe Uhuru pekee
Ili tuweze kusema Uhuru ndiye kiongozi wa serikali, haujanisikia nikilalamika, hali yangu na rais imekubaliwa." Aliongea Ruto.
Huku akizungumzia utata ulio katika chama hicho Ruto alisema kuwa muda upo wa kusuluhisha matatizo hayo na iwapo suluhu haitapatikana ataweza kuruka nje.
"Matatizo ni ya viongozi kutatua. Hatuwezi kupotea, lakini ikishidikana kuna namna nyingi kwa siasa. Kwa mfano wakati mheshimiwa rais aliona kuna matatizo mengi aliunda chama cha TNA
Mimi pia wakati niliona chama cha ODM kimekuwa na udikteta, niliamua vingine. Lakini naamini bado hatujafika kuamua vingine."
Mimi pia wakati niliona chama cha ODM kimekuwa na udikteta, niliamua vingine. Lakini naamini bado hatujafika kuamua vingine."
