logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wabunge wamtolea Maraga makucha kuhusu ushauri wake wa kulivunja bunge

Wabunge wamtolea Maraga makucha kuhusu ushauri wake wa kulivunja bunge

image
na

Habari01 October 2020 - 09:22
Kioni
Kamati moja ya bunge sasa inamtaka mkuu wa  jaji mkuu David Maraga kufika bunge ili kutoa maelezo kuhusu ushauri wake kwa rais kwamba bunge livunjiliwe mbali .

Kamati ya kusimamia utekelezaji wa katiba inayoongozwa na  Jermiah Kioni imesema ilikuwa makosa kwa maraga  kulishtumu bunge kwa kukosa kutekeleza sharia ya usawa wa kijinsia ilhali hata idara ya mahakama  haijatekeleza kanuni hiyo .

Awali  tume ya utumishi kwa bunge PSC  ilisema itachukua hatua ya kupinga ushauri wa Maraga kwa rais Kenyatta .

Mwenyekiti wa PSC spika wa bunge Justin Muturi  amesema ushauri huo haufai ni unakiuka katiba .

Amesema tume hiyo inajutia kwamba jaji Mkuu anatishia kulitumbukiza taifa katika mgogoro wa kikatiba  bila kutumia busara  na heshima  ya afsisi yake.

Muturi  siku ya jumatatu alisema bunge halifai kufanywa  bagi la kupigwa makonde  akisema sio  jambo linalowezeka kumtaka rais alivunjie mbali bunge kwa kukataa kuteleleza sharia ya usawa wa kijnsia


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved