logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Mungu alipatanisha uhusiano wetu,'Size 8 azungumza baada ya drama yao

usiano wao ulipatanishwa na Mungu ambaye ni Mungu wa patanisho.Huku mashabiki

image
na Radio Jambo

Habari14 October 2020 - 10:45

Muhtasari


•Mungu alipatanisha uhusiano wetu, ni Mungu wa patanisho size 8 azungumzia uhusiano wake na mumewe

•Wacha Mungu akasifiwe kwa upatanisho wake kupitia mwanawe yesu Kristo

Kwa siku chache zilizopita familia ya The Muraya's imekuwa kwenye vichwa vya habari baada ya mumewe msanii wa nyimbo za injili Size 8 DJ Mo kusemekana ya kwamba alimdanganya mkewe na kutoka nje ya ndoa.

Mengi yalisemwa huku Size 8 akikiri kuwa alifurahi ya kwamba Mo alijiondoa katika ndoa yao, huku Mo naye akimwambia mkewe kuwa ni wake milele.

Huku akisherehekea ndoa yao, kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram Size 8 alisema ya kwamba uhusiano wao ulipatanishwa na Mungu ambaye ni Mungu wa patanisho.

 

Huku mashabiki wake wakijibu ujumbe wake wengi waliwashauri wengine wasiweze kuwaamni watu mashuhuri au ukipenda macelebs kwa mambo ambayo wanafanya.

Huu hapa ujumbe wa Size 8;

"Mungu alipatanisha uhusiano wetu kupitia kwake mwanawe yesu kristo mkombozi wetu na ndio juhudi zake mwenyezi Mungu hazibadiliki

Anapatanisha mahusiano kupitia neema ambayo aliimwaga duniani kupitia Yesu Kristo." Aliandika Size 8.

Huku akiendelea na ujumbe wake alisema kuwa Mungu na atukuzwe kwa patanisho yake na uzuri wake.

"Tazama uweza wa Mungu wa upatanisho ulioonyeshwa kwa ulimwengu kuona,wacha jina lake Mungu likasifiwe, nisaidieni kumsifu Mungu wa patanisho."

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved