logo

NOW ON AIR

Listen in Live

PATANISHO:Mke wangu alitolewa kwa ndoa na dada yake

nitashukuru uamuzi wake, kwa maana mimi nampenda sana na moyo wangu wote.

image
na Radio Jambo

Habari19 October 2020 - 05:36

Muhtasari


  • Mke wangu alitolewa katika ndoa yetu na dada yake
  • Mimi simpendi Ken na sitaki kuzungumza naye
  • Mimi nimemfungulia njia kwa wale wote walikuwa wanadhani niko nayo pia mimi nimerudi kwa kiwanja

Bwana Ken alituma ujumbe studioni zetu ili apatanishwe na mke wake Croline ambaye wamekuwa kwa ndoa kwa miaka sita ilhali dada yake alimshawishi atoke katika ndoa yake mwaka jana Oktoba.

"Tumekuwa kwa ndoa kwa miaka sita, mimi na mke wanhu huwa tunakosana kwa sababu ya shida za kinyumbani lakini tunasuluhisha

Mwaka jana dada yake alimwambia atoke kwenye ndoa, nahisi kuwa dadake hanipendi, lakini nahisi mke wangu bado ananipenda

 

nataka kujua kama ile upendo alikuwa nao nilipomuoa,nataka aniambie mbele ya wakenya kama hanipendi ama ananipenda

nitashukuru uamuzi wake, kwa maana mimi nampenda sana na moyo wangu wote." Alieleza Ken.

Tulipofanya juhudi zetu za kumfikia Mkewe Caroline Chebet alikuwa na haya ya kusema,

"Mimi sitaki kuzungumza naye na simpendi kabisa." Caroline Alisema.

Baada ya kuzungumza hayo Ken alisema kuwa wamebarikiwa na mtoto mmoja ambaye anaishi na mama yake ken.

Je utampa ushauri upi kuhusu mtoto wake?


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved