logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kinara wa ODM Raila Odinga awashtumu wanaopinga BBI

Kiongozi wa ODM Raila Odinga amewashtumu wale wanaopinga BBI akisema kuwa ripoti hiyo haikusudiwa kuhakikisha kuwa anakuwa Rais au Waziri Mkuu bali ni kuunda amani na umoja nchini kwa vizazi vijavyo.

image
na Radio Jambo

Habari25 October 2020 - 09:10
raila odinga na Ruto

Kiongozi wa ODM Raila Odinga amewashtumu wale wanaopinga BBI akisema kuwa ripoti hiyo haikusudiwa kuhakikisha kuwa anakuwa Rais au Waziri Mkuu bali ni kuunda amani na umoja nchini kwa vizazi vijavyo.

Amepuuzilia mbali madai kwamba BBI itaongeza mswada wa mapato wa nchi hiyo akisema kwamba waziri mkuu na manaibu wake watachaguliwa kutoka kwa wabunge na hivyo hakutakua na  mzigo wowote kwa mlipa ushuru.

Hata hivyo, mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati amemkashifu kiongozi wa ODM Raila Odinga na watetezi wengine wa BBI kwa kushutumu IEBC kama sehemu ya shida katika kila uchaguzi.

Chebukati anasema Raila na wenzake wanatumia tume hiyo kwa njia isiyo ya haki. Anasema  ripoti ya BBI inapunguza tena faida iliyopatikana kwa miaka mingi kuhusu  usimamizi wa uchaguzi nchini.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved