logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Uzinduzi wa BBI:Naibu rais William Ruto atarajiwa katika ukumbi wa Bomas

Badala yake Ruto alihudhuria mazishi ya mwakilishi wadi wa Huruma

image
na Radio Jambo

Habari26 October 2020 - 07:21

Muhtasari


  • William Ruto atarajiwa kumkaribisha rais wakati wa uzinduzi wa BBI katika ukumbi wa BBI
  • Ruto alisema kwamba BBI yapaswa kuzingatia mwananchi wa kawaida na wala si vyeo vya uongozi
  • Wiki jana Ruto alisusia kuhudhuria mkutano wa rioti ya BBI kaunti ya kisii
Naibu rais William Ruto

Naibu rais William Ruto anatarajiwa katika ukumbi wa Bomas hii leo katika uzinduzi wa BBI ili kumkaribisha rais Uhuru Kenyatta, hii ni baada ya kususia kuhudhuria mkutano wa ripoti ya BBI wiki jana.

Badala yake Ruto alihudhuria mazishi ya mwakilishi wadi wa Huruma aliyeaga dunia kutokana na virusi vya corona.

Hata hivyo Ruto alisema kuwa BBI haipaswi kuzingatia vyeo vya wanasiasa bali yapaswa kuzingatia hali ya mwananchi wa kawaida.

“Reggae itasimama, haitasimma? Itasimama, wawache kiburi bwana. Msituambia ni lazima na msituambia ya kwamba nobody can stop reggae, Kuna mungu mbinguni na kuna wananchi hawa. Kama Mambo ya wananchi hawa haiku kwa BBI, hiyo Reggae itasimama, ama mnasema aje? Hawa watu watajua hajui,

Tumeona BBI imejazwa mambo ya wadosi. Iko na mambo ya Prime Minister, Imperial President na mambo ya vyeo ya wakubwa. Hatuna shida na hiyo lakini lazima kuwe na mambo ya biashara na kazi ya huyu mwanainchi wa hapa chini." Ruto Alisema siku ya Jumapili.

Kwa upande huu mwingine Uhuru na Raila wamewauliza wananchi wa kenya kuunga mKono BBI baada ya kujisomea na kuamua uamuzi wao.

Raia anatarajiwa kuongoza zaidi ya wakenya 6,000 ambao wamealikwa katika uzinduzi wa BBI katika ukumbi wa Bomas.

Kulingana na ratiba ya hafla hiyo ya leo baadhi ya viongozi ambao wanatarajiwa kuzungumza ni naibu mwenye kiti wa kamati ya BBI Adms Oloo na kinara wa ODM Raila Odinga.

Mnamo mwaka wa 2019,Novemba,27 Ruto alikuwa kwenye vichwa vya habari baada ya madai kuwa alitumiwa vibaya wakati wa uzinduzi wa kawaida wa BBI.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved