logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tuko tayari kwa referenda-wabunge wasema baada ya kukutana na Uhuru ,Raila

Rais Uhuru na Odinga wamekutana na wabunge Naivasha

image
na Radio Jambo

Michezo02 November 2020 - 12:27

Muhtasari


 

  •  Rais Uhuru na Odinga wamekutana na wabunge Naivasha 
  • Orengo  amesema wako tayaro kuunga mkono mapendekezo katika BBI 

 

 Wabunge  wanaowaunga mkono rais Uhuru Kenyatta na kiongozi wa ODM Raila Odinga wamesema wako tayari kwa kura ya maoni kuhusu mapendekezo ya ripoti ya BBI .

 Wajumbe hao kutoka senate na bunge la kitaifa wamesema  wametathmini yaliyomo katoika ripoti hiyo na kuamua kuiunga mkono .

 Hii ni baada ya wabunge hao kufanya kutano na  rais Uhuru na kiongozi wa ODM Raila huko Naivasha .

 Wakiongoziwa na seneta wa Siaya James Orengo ,viongozi hao wamesema wako tayari kulisaidia taifa kuafikia umoja  ambao unahimizwa kupitia mapendekezo ya BBI .

 Amesema kupitia kuongezwa kwa fedha za kaunti hadi asilimia 35  ,kaunti  zitakuwa na raslimaliza kutosha kutoa huduma kwa wananchi .

 Oreng  amesema mswada wa BBI utahakikisha kwamba kesi za uhalifu wa kiuchumi na ufisadi zinashughulikiwa  ndani ya kipindi cha miezi  sita .

 Orengo amesema mkutano wao umeunga mkono pendekezo la kuunda nafasi zaidi za uakilishi ili kukimu mahitaji ya wanawake ,vijana na makundi yaliyotengwa .

" Tuko tayari kuendelea na jitihada za kuhakikisha kwamba kilele chake ni kuandaliwa  kwa kura ya maoni’ amesema Orengo .

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved