logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Vijana,18,wakamatwa wakifanya sherehe Kahawa Sukari

Kulingana na polisi vijana hao walikuwa kati ya miaka 16 na 18

image
na Radio Jambo

Yanayojiri28 November 2020 - 09:49

Muhtasari


  • Vijana,18,wakamatwa wakifanya sherehe Kahawa Sukari
  • Vijana hao walikuwa wanasheherekea siku ya kuzaliwa ya mmoja wao huku wakibugua vileo

Vijana,18,walikamatwa na polisi katika kaunti ya Kiambu huku wakufanya sherehe kinyume cha kanuni za virusi vya covid-19.

Kulingana na polisi vijana hao walikuwa kati ya miaka 16 na 18 walikuwa wanasheherekea siku ya kuzaliwa na mmoja wao ambapo walikuwa wanabugia vileo.

Kulingana na citizen Digital, DCC wa Ruiru Githinji Geoffrey  alisema kwamba vijana hao walikuwa wamekusanyika eneo hilo kinyume na kanuni za wizara ya afya na waliowauzia pombe watakamatwa.

 

Pia aliwauliza wazazi wawe makini na mahali watoto wao wako hasa wakati huu shule zimefungwa na asilmia kubwa ya wanafunzi wako nyumbani.

DCC Githinji alisema kuwa watoto hao wataachiliwa kwa wazazi wao mnmo siku ya Jumamosi.

Haya yanajiri siku chache baada ya vijana zaii ya arobaini kukamatwa wakiwa wamefungiwa nyumbani na wakibugia vileo huku polisi wakipata kondomu zilizotumiwa.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved