logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Cheza na malaika nakupenda sana,'Mpenzi wake Shanti aomboleza

Ni tamasha ambayo ilikuwa imeandaliwa na mwanasosholaiti Bridget Achieng.

image
na Radio Jambo

Habari30 November 2020 - 11:11

Muhtasari


  • Shanty alichapwa na walinzi lango katika tamasha ya Nai Fest iliyokuwa imeandaliwa na Bridget Achieng
  • Mpenzi wake alimuomboleza kwa ujube wenye huzuni

Jamaa,familia na marafiki wa Steven Munga almaarufu hawajaweza kuamini kuwa ameaga dunia kutokana na kichapo ambacho alipokea kutoka kwa walinzi mlango katika tamasha la Nai Fest tarehe 7,Novemba.

Ni tamasha ambayo ilikuwa imeandaliwa na mwanasosholaiti Bridget Achieng.

Kijana huyo ambaye alikuwa mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule ya upili ya Mukaa hakurejea nyumbani kwao siku hiyo huku simu yake ikizimwa.

Kulingana na mpasho mwili wake ulipatikana kwenye kuchamba cha kuifadhi maiti siku tano baadae.

"Tumekuwa tukimtafuta kwa siku tatu, tumeenda katika vituo vya polisi kadhaa, hospitali na hata vyumba vya kuifadhi maiti

Tulimpata baadaye katika chumba cha kuifadhi maiti jijini Nairobi, kichwa chake kilikuwa kimebondwa na jicho lake limedungwa."Baba yake aliambia vyombo vya habari

Kupitia kwenye mitandao ya kijamii mpenzi wake aliandika ujumbe wa kumuomboleza huku akisema kwamba anampenda sana.

"Nakupenda sana, cheza na malaika huko juu 🥺🥺RIP…" Aliandika mpenzi wake Shanty.

kupitia katika posti nyingine aliandika,

"RIP BABE😪😪."

 

Pia baba yake alisema kwamba marafiki zake waliokuwa nao walisema kwamba alirudi bila shati na viatu vyake, hii ni baada ya kuambiwa kuwa yeye ni mwizi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved