Wanamitandao walijawa na hasira na ghadhabu baada ya msanii Bahati na mkewe Diana Marua kufichua kuwa hawakuwa wameachana badala yake walikuwa wanatafuta kiki.
Wawili hao walikuwa wanajiandaa kutoa kibao kipya ambacho kinafahamika kama 'Mtaachana tu'.
Wiki jana na mapema wiki hii wawili hao walikuwa kwenye vichwa vya habari na hata kuenea sana kwenye mitandao ya kijamii baada ya uvumi kuene kuwa wawili hao wameachana.
Kwenye mitandao ya kijamii ya twitter wanamitandao walimkashifu bahati vikali sana kwa kitendo hicho huku wengine wakisema kuwa ni njia moja wapo ya wasanii kufanya nyimbo zao kupendwa na mashabiki.
Kupitia kwenye kibao hicho kimeelekezewa wakejeli ambao huwa wanasema wawili hao wataachana.
Pia wanazungumzia jinsi wawili hao wataishi pamoja licha ya watu kusema wataachana.
Hizi hapa baadhi ya hisia za wanamitandao kuhusu tendo hilo;
Cyprian is Nyakundi: Rehabilitated chokoraa Bahati who sings the shittiest songs in this country, together with his brand new second-hand wife Diana, faked a break up just to chase clout. Kenyans should start boycotting these childish stunts.
Cyprian Ongeri: "Rehabilitated chokoraa" and his "brand new second-hand wife"... πππ Mlisema hii app hakuna amani kabisa...
Mathenge Wahome: Told you that you were chasing clout ona sasa, just concentrate on music
