logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Otile Brown hatimaye azungumza baada ya Octopizzo kuwakashifu wakenya

"Sadieni msanii ambaye mnataka, unga mkono chochote ambacho unataka na unapenda

image
na Radio Jambo

Habari11 December 2020 - 09:54

Muhtasari


  • Otile Brown azungumza baada ya Octopizzo kuwakashifu wakenya kwa kumuunga mkono Diamond

Siku chache baada ya msanii Diamond kutoa kibao chake kipya cha 'Waah' wakenya walimuunga mkono huku rappa Octopizzo akighadhabishwa na kitendo hichona hata kuwakashifu.

Siku chache baada ya ukashifu wake Otile Brown ameweza kuzungumza na kusema kila mtu ana haki ya kuunga na kupenda kibao ambacho anataka au msanii ambaye anataka.

Kupitia kwenye ukrasa wake wa twitter Otile alikuwa na haya ya kusema;

 

"Sadieni msanii ambaye mnataka, unga mkono chochote ambacho unataka na unapenda, muziki hauna mipaka, wivu ni ishara ya udhaifu na sio yetu

ata ukitaka leta ushindani wako chini, huwezi lazimisha watu wapenda ujinga wako, sina jambo lolote dhidi ya wasanii wa humu ata wanchi za nje ni upendo tu

Wakati mwingine naweza kuwachukia laini si jambo la kibinafsi, hii ni burudani tu, ndugu yetu anastahili hili alifanyia kazi haya

Ninaheshimu wasanii wote licha ya nyimbo zipi wanaimba, kama inaleta pesa basi ni sawa, tuwache kunung'unika kibuma turudi jikoni kwa vyombo vyetu vya habari endeleeni kutuunga mkono

Si tu wasanii wale maarufu zaidi au nyimbo kali..kama wimbo ni mzuri peana shavu ata kama ni msanii chipukizi

Ni sawa kamahautapenda muziki wangu au kuunga mkono." Otile Brown Aliandika.

 

 

 

 

 

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved