Halmashauri ya kukadiria ubora wa bidhaa KEBS imeidhinisha viwango vya ubora vitakavyotumiwa kuongoza uzalishaji wa wadudu wanaoliwa na bidhaa zinazotokana na wadudu hao .
Viwango hivyo vya ubora KS 2921:2020 vimetoa mahitaji ambayo yanafaa kutoshelezwa na wakulima ikiwemo hali itakayofanikisha uzalishaji na uuzaji wa wadudu hao ili kutumiwa kama chakula . Pia vinatoa kiwango kinachohitajika cha miundo msingi inayohitajika kwa uzalishaji wa wadudu kwa wingi .
Maneja mkurugenzi wa KEBS Bernard Njiraini amesema KS 2922 Part 1 ni mwongozo utakaoeleza na kuratibu mahitaji ya kupakiwa na kuuzwa kwa wadudu hao wakiwa wazima ama wakisagwa .
KS 2922 Part 2 ni mwongozo utakaotumika kuunda bidhaa zinazotokana na wadudu hao kama vile biskuti na bidhaa nyingine .