logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wilbroda afichua sababu ya kutembelea familia ya Papa Shirandula

Hii ni baada ya marafiki hao kutembelea familia yake katika kaunti ya Busia.

image
na Radio Jambo

Dakia-udaku14 December 2020 - 02:47

Muhtasari


  • Muigizaji Wilbroda aeleza sababu yao kuenda kutembelea familia ya papa shirandula miezi chache baada ya mazishi yake
Papa-Shirandula-Wilbroda-696x418

Wikendi iliyopita marafiki wake mwendazake Charles Bukeko almaarufu Papa Shirandula wikendi iliyopita walisheherekea sikukuu ya Jamhuri kwa njia ya kipekee.

Hii ni baada ya marafiki hao kutembelea familia yake katika kaunti ya Busia.

Wengi hawakufahamu sababu ya marafiki hao kuenda eneo hilo bali aliyekuwa muigizaji wa kipindi hicho Jackline Nyaminde almaarufu kupitia kwenye ukurasa wake alifichua sababu ya wao kuenda huko.

 

Huku akipakia picha ya Njoro,Awinja naye liandika ujumbe huu;

" Ni wikend ya ajabu aje, kurudi Nanderema, Samia kaunti ya Busia kutembelea familia ya Papa na wazazi wake na eneo ambalo tulimzika

Kijiji chote kilikua na nilisikia vizuri, ilikuwa sherehe,tuliimba,tukasakata densi, tukakula na tukakunywa ni ahadi ambayo tulifanya wakati wa mazishi yake tutarudi tena

Tunafuraha kwa maana tulitimiza ahadi hiyo, wazazi wake na familia yake walijawa na furaha na mioyo yetu ilikuwa imejaa." Aliandika Wilbroda.

Wakati huo huo muigizaji mwenzake Jacy Vike almaarufu Awinja alimtambulisha nduguye Papa kwa mashaibiki.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved