logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wakenya wanajua nani mnyakuzi wa ardhi,'Ngilu amtetea Kalonzo

"Madai ya Ruto kwamba Kalonzo alinyakua ardhi ni uongo,

image
na Radio Jambo

Habari19 January 2021 - 14:20

Muhtasari


  • Charity Ngilu amtetea Kalonzo dhidi ya madai yake DP Ruto kwamba amenyakua ardi ya NYS
  • Akizungumza siku ya Jumanne alisema kwamba kila mkenya anafahamu mnyakuzi wa ardhi ni nani
  • Pia alisisitiza kwamba Kalonzo alinyakua ardhi hiyo kisheria

Gavana wa kaunti ya kitui Charity Ngilu amemtetea kinara wa chama cha Wiper Kalonzo Musyoka kutokana na  madai yake naibu rais William Ruto.

Kulingana na Ngilu DP hana jukwaa la maadili kumfundisha mtu yeyote juu ya maswala ya unyakuzi wa ardhi.

"Madai ya Ruto kwamba Kalonzo alinyakua ardhi ni uongo, kila mkenya anaweza kutambua na kujua nani mnyakuzi mkubwa wa ardhini nani katika nchi yetu kama si duniani." Ngilu alizungumza.

 
 

Wiki jana DP Ruto alidai kwamba kalonzo amenyakua ardhi ya hekari 200 katika eneo la Yatta ni shamba ambayo ilikuwa ni ya National Youth Service.

Ngilu alisisitiza kwamba Kalonzo alichukua ardhi hiyo kupitia kwa sheria.

Kalonzo pia alikana madai hayo na kusema kwamba yuko tayari kuchunguzwa na kuhojiwa kwa ajili ya shamba hilo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved