logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Lupita Nyong'o amkejeli CS Balala baada ya kusema hawakumpata kwa miaka 5

Waziri wa Utalii Najib Balala alisema haya baada ya kulazimishwa kutetea uteuzi

image
na Radio Jambo

Habari22 January 2021 - 12:37

Muhtasari


  • Lupita acheka madai yake waziri wa utalii Balala
  • Balala alisema kuwa wamekuwa wakimtafuta Lupita kwa miaka mitano

Mwigizaji wa Kenya aliyeshinda tuzo tofauti Lupita Nyong’o amecheka madai kwamba Kenya imekuwa ikimtafuta kwa miaka mitano.

Waziri wa Utalii Najib Balala alisema haya baada ya kulazimishwa kutetea uteuzi wa hivi karibuni wa supermodel Naomi Campbell kama balozi wa kimataifa wa Magical Kenya badala ya Lupita.

Balala aliliambia Nation kwamba wizara yake ilijaribu kuwasiliana bila mafanikio na Lupita kwa miaka mitano sasa.

“Najua kila mtu anauliza kwanini asiulize Lupita. Lupita ana ahadi na mameneja wake hawawezi kuturuhusu kumfikia. Tumetumia miaka mitano iliyopita kumtafuta Lupita." Balal Alisema.

Baada ya kuona na kusikia madai yake Balala Lupita alipakia picha kwenye ukurasa wake watwitter huku akicheka madai yake Balala.

"Mimi nikisikia Wizara ya Utalii ya Kenya imekuwa ikinitafuta kwa miaka mitano. #Imrightherebaby #alternativefacts." Aliandika Lupita.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved