logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ni rangi ambayo amepaka nywele inaathiri akili yake?Shakilla amshambulia msanii Vivian baada ya kusema haya

Hivi majuzi alimkejeli Mejja kwa kuwa mmoja wa wasanii ambao waliimba kibao cha 'Nairobi'

image
na Radio Jambo

Habari22 January 2021 - 21:25

Muhtasari


  • Shakilla amshambulia msanii Vivian baada ya kusema kuwa ni mpenzi wa siri wa Mejja
vivian musician

Mwanasosholaiti chipukiza Shakilla anafahamika kwa mambo mengi ambayo amekuwa aitenda na kusema kwenye mitandao ya kijamii.

Hivi majuzi alimkejeli Mejja kwa kuwa mmoja wa wasanii ambao waliimba kibao cha 'Nairobi' chake msanii Bensoul.

Huku msanii Viviana akitoa maoni yake kuhusu matamshi yake Shakilla alikuwa na haya ya kusema;

 

"Niliona habari mitandaoni kuhusu Shakilla, ambaye alimkejeli Mejja baada ya kibao cha Nairobi kutoka,kati ya wasanii wote ambao walikuwa kwenye kibao hicho aliona Mejja

Ama umempenda kwa siri, kama unataka nikuunganishe naye kuja kwangu Mejja ni rafiki yangu." Vivian Alimwambia mwanasosholaiti huyo.

Baada ya Shakila kuona video yake msanii Vivian alipakia video hiyo kwenye ukurasa wake wa instagram na kuandika ujumbe akiwa amempa maneno makali.

"2021 si mitaani mniambia nitafanyia nini huyu, ni rangi ambayo amepaka nywele zake inaathiri akili yake kuwa na ujasiri wa kuniambia hivo

Malkia wa mitaa mimi niwe mpenzi wa siri." Shakilla Aliuliza.

Je drama hii itaendelea mpaka lini?


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logoΒ© Radio Jambo 2024. All rights reserved