logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Majimbo Kalasinga wa Ford Kenya anyakua kiti cha Kabuchai

Majimbo Kalasinga wa Ford Kenya anyakua kiti cha Kabuchai

image
na Radio Jambo

Burudani05 March 2021 - 04:21

Muhtasari


• Kalasinga alizoa jumla ya kura 19,274 kubwaga wenzake katika uchaguzi huo ambao ulikumbwa na visa kadhaa vya ghasia.

• Kulingana na tawimu za IEBC ni asilimia  51.68 ya watu waliojitokeza kushiriki uchaguzi huo.

Majimbo Kalasinga aonyesha cheti baada ya kutangazwa mshindi wa kiti cha eneo bunge la Kabuchai ameandamana na kinara wa Fork Kenya Moses Wetangula.

Simiyu Majimbo Kalasinga wa chama cha Ford Kenya ametangazwa mshindi wa uchaguzi mdogo wa kiti cha eneo la Kabuchai.

Kalasinga alizoa jumla ya kura 19,274 kubwaga wenzake katika uchaguzi huo ambao ulikumbwa na visa kadhaa vya ghasia.

Afisa wa IEBC aliyesimamia uchaguzi huo Benson Esuza alimkabidhi Majimbo cheti Ijumaa asubuhi. 

 

Mgombeaji wa chama cha UDA ambaye alikuwa anapigiwa debe na wandani wa naibu rais William Ruto Evans Kaikai alikuwa wa pili kwa kupata kura 6,455. Wengine waliowania kiti hicho ni  Wekesa Amos Wafula wa FPK na kura 1, 454, Waffubwa Gasper Mufutu, mgombeaji huru alipata kura 1,236.

Kulingana na tawimu za IEBC ni asilimia  51.68 ya watu waliojitokeza kushiriki uchaguzi huo.

Katika chaguzi zingine zilizofanyika siku ya Alhamisi, chama cha Wiper kilishinda kiti cha wadi ya Kitise/Kithuki katika kaunti ya Makueni.  Mgombeaji wa Wiper Sebastian Muli Munguti alipata kura 3,892 kumbwaga mpinzani wake wa karibu Joseph Kioko wa chama cha Muungano aliyepata kura 878.

Kioko ambaye alimaliza wa pili alikuwa akipigiwa debe na gavana wa Makueni Kivutha Kibwana.

Kiti hicho kilivutia wagombeaji saba.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved