logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Afueni kwa wenye mikopo ya benki, CBK yaongeza muda wa kulipa

Afueni kwa wenye mikopo ya benki, CBK yaongeza muda wa kulipa

image
na Radio Jambo

Habari23 March 2021 - 07:28

Muhtasari


  • Wenye mikopo ya benki sasa wana miezi mitatu ya ziada kuanza kulipia hiyo baada ya Benki Kuu ya Kenya kuongeza muda huo hadi Julai 3.

Gavana wa Benki Kuu ya Kenya Patrick Njoroge

Wenye mikopo ya benki sasa wana miezi mitatu ya ziada kuanza kulipia hiyo baada ya Benki Kuu ya Kenya kuongeza muda huo hadi Julai 3.

Katika taarifa iliyotolewa siku ya Jumanne, Benki Kuu ya Kenya ilisema kwamba agizo hili linahusu tu mikopo ambayo ilikuwa ikilipiwa kufikia Machi 2, 2020 lakini ikaingia kwenye malimbikizo baadaye kutokana na athari za janga la Covid-19.

'' CBK itaendelea kufuatilia kwa karibu kufutwa kwa mikopo iliyobadilishwa ili kuhakikisha uthabiti wa sekta ya benki, '' CBK ilisema.

Benki kuu ilifichau kwamba angalau mikopo yenye thamani ya Shilingi trilioni 1.7, inayowakilisha asilimia 57 ya jumla ya mikopo ya benki ili fanyiwa mabadiliko katika mikaba yake ya ulipaji tangu ilipotangaza hatua ya dharura katikati mwa mwezi Machi mwaka jana ili kuwaokoa akopaji kutokana athari za janga la Covid-19.

Hata hivyo, tangu kulegezwa kwa masharti ya udhibiti wa maambukizi ya virusi vya corona, wakopaji walianza kulipia mikopo, na kupunguza mikopo iliyobadilishwa hadi shilingi bilioni 569.3 au asilimia 19.

Angalau asilimia 95 ya wakopaji sasa wanalipia mikopo yao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved