Shirika la Ndege nchini (Kenya Airways) siku ya Jumanne lilitangaza kusajili hasara ya jumla ya Shilingi bilioni 36.57 katika kipindi cha fedha cha mwaka jana.
Hasara iliyosajiliwa na kampuni hiyo iliyongezeka mara tatu zaidi ya hasara iliyosajiliwa kipindi cha mwaka uliyotangulia.
Ingawa kampuni ya KQ imekuwa ikikabiliwa na changamoto za kifedha, hali yake iliathirika zaidi kutokana na janga Covid-19, lililopelekea kusitishwa kwa safari zote za ndege kwa kipindi kirefu mwaka uliyopita.
KQ ambayo inamilikiwa kwa kiasi fulani na kampuni ya Air France KLM, ilisema mapato yake yalitumbukizwa zaidi ya nusu katika kipindi cha mwaka jana, baada ya kusitishwa kwa safari za ndege.
Afisa mkuu mtendaji wa shirika hilo ndege Allan Kilavuka alisema idadi ya abiria ilipungua sana wakati wa kipindi cha fedha cha mwaka jana hadi milioni 1.8 ikilinganishwa na milioni 5.2 mwaka 2019.
Hali hii ilisababisha kupungua kwa mauzo ya KQ kwa asilimia 60 hadi Shilingi bilioni 52.