logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Magoha aonya walimu wakuu dhidi ya kuwachanganya watahiniwa

Magoha aonya walimu wakuu dhidi ya kuwachanganya watahiniwa

image
na Radio Jambo

Habari07 April 2021 - 07:46

Muhtasari


• Waziri alisema kwamba walimu hao wakuu wamekuwa wakiwachanganya wanafunzi kwa kuwafanya kudurusu karatasi bandia na kukumbana na maswali tofauti.

• Kufikia Jumanne, serikali ilikuwa imechukua zaidi ya vifaa 832 vya kigeni katika vituo vya mitihani ikiwa ni pamoja na simu za rununu na karatasi bandia.

Waziri wa elimu George Magoha amewashauri wasimamizi wa vituo vya kufanyia mtihani kutokuwa walafi na kununua karatasi gushi za mtihani wa KCSE.

Magoha siku ya Jumatano alisema kwamba serikali imegundua kuwa baadhi ya wakuu wa shule ambao ndio mameneja wa vituo vya kufanyia mtihani wamekuwa wakifanya jitihada kushiriki udanganyifu wa mitihani.

Waziri alisema kwamba walimu hao wakuu wamekuwa wakiwachanganya wanafunzi kwa kuwafanya kudurusu karatasi bandia na kukumbana na maswali tofauti wanapoingia katika chumba cha mtihani.

 

Magoha aliwahakikishia wakenya kuwa serikali imejitolea kuhakikisha kwamba mitihani yote inalindwa  na kwamba hakuna karatasi inayovuja.

Kulingana na waziri, hakuna karatasi halisi ya mtihani iliovuja, akisema kwamba tayari wameratibu maeneo ambapo majaribio ya wizi wa mitihani yamekithiri.

"Mitihani imekuwa ikiendelea vizuri kote nchini hadi watu wengine walipoanza kuwachanganya watoto kwa kuwapa karatasi bandia. Wasimamizi wa vituo pia walisambaza karatasi hizo bandia kwenye mtandao," Magoha alisema.

Akizungunza siku ya Jumatano alipoongoza zoezi la kusambaza mitihani mjini Homa Bay waziri alihimiza maafisa wa usalama kutolegeza kamba katika kudumisha usalama wa mitihani.

Wasimamizi wa mitihani walihimizwa kufanya uhakiki kamili na kupiga msasa watahiniwa ili kuwazuia kuingia kwenye chumba cha mitihani na vifaa visivyo ruhusiwa.

 

Kufikia Jumanne, serikali ilikuwa imechukua zaidi ya vifaa 832 vya kigeni katika vituo vya mitihani ikiwa ni pamoja na simu za rununu na karatasi bandia.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved