logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Baraza la Habari Kenya lataka uchunguzi wa haraka katika mauaji ya mwanahabari Betty Barasa

Hadi kifo chake, Betty alikuwa mhariri mwandamizi wa video katika Shirika la Utangazaji la KBC.

image
na Radio Jambo

Habari08 April 2021 - 11:19

Muhtasari


  • MCK yataka uchunguzi wa haraka katika mauaji ya mwanahabari Betty Barasa
  • Baraza la Habari Kenya limelaani mauaji ya mwandishi wa habari Betty Barasa, yaliyotokea usiku wa kuamkia leo
  • Hadi kifo chake, Betty alikuwa mhariri mwandamizi wa video katika Shirika la Utangazaji la KBC

Baraza la Habari Kenya limelaani mauaji ya mwandishi wa habari Betty Barasa, yaliyotokea usiku wa kuamkia leo.

Hadi kifo chake, Betty alikuwa mhariri mwandamizi wa video katika Shirika la Utangazaji la KBC.

Aliuawa kwa kupigwa risasi akiwa nyumbani kwake huko Ngong, eneo la Ololua wakati wa wizi.

Alikuwa amewasili nyumbani kwake mwendo wa saa mbili na nusu usiku wakati genge lililokuwa likingojea mlangoni lilijilazimisha kuingia ndani ya boma wakati lango lilipofunguliwa, mashahidi walisema.

Katika taarifa Alhamisi, baraza hilo lilitaka uchunguzi wa haraka kubaini wahusika wa kifo chake.

"Baraza linalaani kitendo hicho cha vurugu ambacho kilisababisha kifo chake kabla ya wakati jana ... ipasavyo, baraza linataka uchunguzi wa haraka juu ya tukio hilo, kwa nia ya kukamata wahalifu na kushtakiwa," MCK alisema.

MCK ilisema kuwa vitendo vya unyanyasaji dhidi ya waandishi wa habari na wafanyakazi wa vyombo vya habari havikubaliki na ni ukiukaji wa uhuru wa vyombo vya habari kama ilivyoonyeshwa chini ya kifungu cha 34 na 35 cha katiba.

Polisi wameanza uchunguzi wa kifo chake. Betty alikuwa amehamia tu nyumbani hivi karibuni.

Kulingana na familia yake, wanaume watatu walikuwa wakimsubiri afike.

Kutoka kwetu wanajambo Mungu azidi kuilaza roho yake mahali pema peponi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved