logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Msichana wa miaka 15 akamatwa kwa kuavya na kutupa vijusi chooni

Msichana wa miaka 15 akamatwa kwa kuavya na kutupa vijusi chooni

image
na Radio Jambo

Habari08 April 2021 - 08:44

Muhtasari


• Mkurugenzi wa DCI George Kinoti alisema wapelelezi waliokoa kijusi kimoja katika hali mbaya baada ya kutupwa katika shimo cha la choo.

• Watoto hao walikimbizwa katika Kituo cha Afya cha Bartabwa huko Kabartonjo, ambapo mmoja alitangazwa kufariki

Msichana wa miaka 15 amekamatwa baada ya kuavya mimba huko Kabartonjo katika kaunti ya Baringo.

Mkurugenzi wa DCI George Kinoti alisema wapelelezi waliokoa kijusi kimoja katika hali mbaya baada ya kutupwa katika shimo cha la choo.

Maafisa ambao walikuwa wamepata ripoti kutoka kwa majirani walifanya haraka kubomoa choo na kuokoa kitoto hicho.

"... walipongia ndani waligundua kwamba kulikuwa na vijusi viwili vilivyokuwa vimezama ndani ya kinyesi cha binadamu," Kinoti alisema.

Watoto hao walikimbizwa katika Kituo cha Afya cha Bartabwa huko Kabartonjo, ambapo mmoja alitangazwa kufariki, wa pili alipelekwa Hospitali ya Rufaa ya Kaunti ya Baringo kwa matibabu maalum.

Mtuhumiwa atashughulikiwa kisheria kulingana na makosa yake.

Kulingana na katiba, kila mtu ana haki ya kuishi na kwamba maisha ya mtu huanza wakati wa kutungwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved