logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hakuna siku watoto wangu walikosa walichotaka,'Mchekeshaji Professor Hamo ajibu madai ya kutowasaidia wanawe

Pia alifichua kwamba mkewe ndiye huwatumia msaada wanawe ambao haishi na wao.

image
na Radio Jambo

Habari02 May 2021 - 07:46

Muhtasari


  • Mchekeshaji Professor Hamo ajibu madai ya kutowasaidia wanawe
  • Jemutai alifichua kwamba walipatana na Hamo kwenye kipindi cha Churchill ambapo walianza uhusiano wa kimapenzi licha ya Hamo kuwa na familia
images

 Mchekeshaji wa churchill Professor Hamo na mcheshi Jumutai wamevuma sana baada ya mwanablogu Edgar kufichua kwamba mchekeshaji huyo hawasaidii wanawe.

Jemutai alifichua kwamba walipatana na Hamo kwenye kipindi cha Churchill ambapo walianza uhusiano wa kimapenzi licha ya Hamo kuwa na familia.

Mcheshi hyo alisema kwamva anahitaji msaada kwani hana pesa za kulipa kodi ya nyumba na baba wa watoto wake hawasaidii.

 
 

KUpitia kwenye ukurasa wake wa instagram wa Hamo,amekana madai hayo na kusema kwamba hamna siku hata moja wanawe walilaal njaa wala kukosa walichohitaji maishani.

Pia alifichua kwamba mkewe ndiye huwatumia msaada wanawe ambao haishi na wao.

"Najua meni yamesemwa lakini nataka kuweka mambo bayana kwa mashabiki wangu, nina watoto ambao naishi nao na ambao hawaishi na mimi

Nimekuwa nikiwasaidia wanangu tangu siku ya kwanza na hamna siku ambayo walikosa chakula wala mahali pa kuishi ama kile walitaka

Mkewe wangu ndiye huwa anatuma pesa kwa watoto ambao hawaishi na sisi, haya yamekuwa makubaliano kati ya familia yangu na mama wa watoto wangu," Alisema Hamo.

Kupitia kwa ujumbe mwingine mchekeshaji huyo alidai kwamba anaamini watoto wanahitaji mazingira yenye utulivvu wanapokua.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved