logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nimewasamehe wale walinitusi,'Msanii Justina Syokau awaambia mashabiki

KUpitia kwenye video iyo, msanii Syokau alidai kwamba amebakisha deni ya milioni 6.7

image
na Radio Jambo

Habari17 May 2021 - 13:34

Muhtasari


  • Msanii wa nyimbo za injili Justina Syokau amekuwa akivuma kwenye mitandao ya kijamii kwa muda sasa baada ya kufichua kwamba anahitaji msaada wa pesa kutoka kwa wakenya

Msanii wa nyimbo za injili Justina Syokau amekuwa akivuma kwenye mitandao ya kijamii kwa muda sasa baada ya kufichua kwamba anahitaji msaada wa pesa kutoka kwa wakenya.

Siku ya JUmatatu kupitia kwenye ukurasa wake wa facebook alipakia video na kusema kwamba amewasamehe wale wote walimtusi alipokuwa anapitia magumu.

PIa aliwashauri na kuwaonya mashabiki kwaba sio vyema kwa mtu kumtusi au kuongea mambaya kuhusu mtu akiwa mgonjwa kwani hawajui wala kufahamu kile wanapitia wakati huo.

Baadhi ya wanamitandao walimkejeli msanii huyo na kumwamboa kwamba anapaswa kuuza mali yake aliyonayo ili apate pesa na awache kuwatapeli wakenya.

KUpitia kwenye video iyo, msanii Syokau alidai kwamba amebakisha deni ya milioni 6.7, huku mashabiki wakizua mjadla mkali kwenye mitandao hiyo.

Pia aliwashukuru mashabiki wake na wale wote ambao wamemshika mkono na kumsaidia,alisema kuwa na ploti lakini hawezi uza kwa bei ya chini kwa maana anahitaji msaada.

"Bwana asifiwe, Mungu awabariki kwa kunishika mkono, asanteni kwa maombi yenu, nimeona watu wakisema na kutoa maoni kwamba natapeli watu

Kuna wale wanasema nifariki,lakini siwezi kufa kwa sasawale wote walinitusi nataka kuwaambia kwamba nimewasamehe

Kama mtu ni mgonjwa na humpendi haya basi usijaribu kumwamndikia matusi kwa maana hujui nini wanapitia, kama hunipendi usiandike kitu mbaya ama wacha kuwa shabiki yangu," Alisema Syokau.

Hii hapa video ya usemi wake;


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved