logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Mimi pekee ndiye tajiri kuliko Diamond" Ringtone adai

Mwanamuziki Ringtone Apoko amemuunga mkono Diamond kuisuta Forbes kwa kutofanya utafiti dhabiti wa wasanii tajiri zaidi AfrIka

image
na Radio Jambo

Habari18 May 2021 - 11:31

Muhtasari


•Ringtone adai kuwa yeye ndiye mwanamuziki tajiri zaidi Afrika Mashariki

•Diamond aliisuta Forbes kwa kumtaja kama nambari ishirini na nane kwenye orodha ya wanamuziki tajiri zaidi Afrika.

Ringtone Apoko

Mwanamuziki wa nyimbo za injili, Alex Apoko almaarufu kama Ringtone amemuunga mkono Diamond kusuta shirika la Forbes.

Diamond aliisuta Forbes kwa kumtaja kama nambari ishirini na nane kwenye orodha ya wanamuziki tajiri mno Afrika.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Ringtone amedai kuwa yeye pekee ndiye amempiku Diamond kwa utajiri eneo la Afrika Mashariki.

Ringtone pia ameiagiza shirika hilo la habari kuwahusisha wasanii wa nyimbo za injili.

Wakati mwingine Forbes shirikisheni wanamuziki wa injili wakati . Msiogope kuniweka kama nambari moja kwani huo ndio ukweli na ukweli utawaweka huru. Diamond ni nambari mbili Afrika iwapo wanamuziki wa injili watashilikishwa.” Ringtone aliandika kwa kiingereza kibovu.

Ringtone alikuja kutambulika zaidi mwakani 2009 baada ya kuwachilia wimbo ‘Pamela’. Ingawaje muziki wake haujakuwa ukivuma sana kw muda mrefu. Amekuwa akihusika kwenye drama si haba.

Rintone hata hivyo hakutajwa kwenye orodha ya wanamuziki thelathini tajiri zaidi Afrika.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved