logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Terence Creative afichua kuwa ananyimwa uwezo wa kuwaona wanawe

Alisema kuwa hajawaona wanawe kwa mda sasa kwani amezuiwa kuwaona. Isitoshe alisema kuwa wanawe wamebadilishwa shule na hilo limefanya mambo kuwa mazito.

image
na Radio Jambo

Habari23 May 2021 - 06:22
Terence.Creative.696x332

Mchekeshaji Terence Creative amewashtua mashabiki wake alipofichua kuwa amenyimwa uwezo wa kuwaona wanawe wawili na aliyekuwa mkewe, Eunice Waneta.

Kwa wale wasiojua, Terence na Eunice Waneta walikuwa kwenye ndoa na walijaliwa watoto wawili wa kike wa miaka 13 na 9 mtawalia.

Terence alifichua haya kwenye kitengo cha maswali na majibu na mashabiki wake katika mtandao wa Instagram.

Alisema kuwa hajawaona wanawe kwa mda sasa kwani amezuiwa kuwaona. Isitoshe alisema kuwa wanawe wamebadilishwa shule na hilo limefanya mambo kuwa mazito.

Mwanzo alikataa kujibu maswali kuhusu wanawe huku akisema ni jambo linalomuumiza moyo, kabla ya kujibu hatimaye.

Shabiki mmoja alipomuuliza kama yeye huwatembelea wanawe alisema;

Okay sawa, mimi huwatembelea shuleni kwa sababu mahali walikuwa wanaishi walihama na sijui wanakoishi saa hii, mmoja alichenjiwa shule yenye nilikuwa najua, saa hii sijui anasomea wapi and the other anasomea Nakuru so nikitaka kumuona lazima niende huko, nauma saana hata baada ya kuwa a good dad and a provider bado nanyimwa shared custody.

Aliongeza;

Katika miaka saba wamekuja kwangu mara moja na kutoka hapo ni stress kabisa kuwaona na ndio maana sipendi kuongelea hii story.

 

0488d0b241d5e30bce81083bec5e4db3

Tazama baadhi ya maswali aliyoulizwa;


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved