logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kuria aondoa mgombeaji wake kwenye kinyang'anyiro cha Kiambaa

Moses Kuria alieleza kuwa uamuzi ulifikiwa baada ya kujadiliana na Ruto, kufurahisha wenzake na kwa umoja wa 'mahustler

image
na Radio Jambo

Habari24 May 2021 - 06:00

Muhtasari


•Moses Kuria alieleza kuwa uamuzi ulifikiwa  baada ya kujadiliana na Ruto, kufurahisha wenzake na kwa umoja wa 'mahustler

•Chama cha PEP kilikuwa kimemteua Raymond Kuria kama mgombeaji wake

Mgombeaji Raymond Kuria wa PEP

Chama cha People’s Empowerment Party(PEP) kinachoongozwa na Moses Kuria kimemuondoa mgombeaji wake kwenye uchaguzi mdogo wa eneo bunge la Kiambaa, Raymond Kuria.

Kupitia ujumbe aliouchapisha kwenye mtandao wa Facebook, mbunge wa Gatundu Kusini alitangaza kuwa uamuzi huo baada ya kukutana na kujadiliana na naibu rais William Ruto.

“Tulijadiliana na mkubwa wangu mtukufu naibu rais William Ruto jana kuhusiana na jambo hili. Ili kuwafanya wenzangu wafurahie na kwa umoja wa muungano wa mahasla, chama cha PEP hakitateua mgombeaji kwenye uchaguzi wa Kiambaa” Kuria alisema.

ujumbe wa moses kuria

Kuria alieleza kuwa uamuzi wa chama cha PEP kuteua mgombeaji haukuchukuliwa vizuri  na baadhi ya wenzake wa Tangatanga huku akitaja haswa Rigathi Gachagua wa Mathira na Kimani Ichungwa wa Kikuyu. Kuria alikuwa amekashifiwa sana kwani chama cha UDA ambacho pia kinahusishwa na naibu rais kilikuwa kimeteua John Njuguna kama mgombeaji wake.

Mbunge huyo ambaye ni mwandani mkuu wa naibu rais alimuomba msamaha Raymond Kuria ambaye alikuwa ashatangazwa kwamba angewania kiti na tikiti ya chama hiyo, watu wa Kiambaa na wanachama wa chama cha PEP akidai kuwa wangesitikishwa na tangazo hilo.

Kuria alisisitiza kuwa nia ya chama cha PEP ilikuwa kuwapa ujumbe wa matumaini na uzinduo mpya wakazi wa Kiambaa. Alisema kuwa chama hicho kinaongozwa na watu wa kawaida haswa vijana ilhali chama cha UDA kinaongozwa na wabunge walio madarakani.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved