logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Ni dhahiri ana shida,'Mwanasiasa Alinur ajitolea kumsaidia msanii Embarambamba

Msanii Embarambamba ambaye anavuma sana kwenye mitandao ya kijamii, amekuwa akipokea kejeli nyingi

image
na Radio Jambo

Habari25 May 2021 - 12:09

Muhtasari


  • Mwanasiasa Honalinur ajitolea kumsaidia msanii Embarambamba
  • Ni tabia ya wakenya na wanamitandao kumuhukumu mtu bila ya kujua kile anachopitia na sababu ya kufanya jambo fulani

Habari njema kwa msanii Embarambamba na mashabiki wake baada ya mwanasiasa Honalinur kujitolea kumsaidia kwa ajili ya kazi yake.

Ni tabia ya wakenya na wanamitandao kumuhukumu mtu bila ya kujua kile anachopitia na sababu ya kufanya jambo fulani.

Msanii Embarambamba ambaye anavuma sana kwenye mitandao ya kijamii, amekuwa akipokea kejeli nyingi sana huku baadhi ya wanamitandao wakidai kwamba hana akili timamu.

Licha ya wakenya wengi kumkejeli Embarambamba baada ya video yake akisakata densi, mwanasiasa huyo amemtetea na kusema atamsaidia.

"Tofauti na watu wengi sitaenda kuketi kiti cha nyuma na kulaani Embarambamba bila kumpa msaada wowote.

Ni dhahiri ana shida. Sasa kazi yake imekufa nusu. Anahitaji msaada haraka au tutapoteza talanta hii adimu. Nitamtafuta na kumsaidia mara moja," Alise,ma Honalinur.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved