logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Covid-19:Watu 344 wapatikana na corona huku 16 wakipoteza maisha yao

Kufikia sasa Kenya imesajili jumla ya visa 170,041kutoka kwa sampuli 1,801,449.

image
na Radio Jambo

Habari28 May 2021 - 13:16

Muhtasari


  • Kenya siku ya Ijumaa  imerekodi visa 344 vipya vya maambukizi ya COVID-19 kutoka kwa sampuli 4,864
  • Kufikia sasa Kenya imesajili jumla ya visa 170,041 kutoka kwa sampuli 1,801,449

Kenya siku ya Ijumaa  imerekodi visa 344 vipya vya maambukizi ya COVID-19 kutoka kwa sampuli 4,864 katika muda wa saa 24 zilizopita.

Kufikia sasa Kenya imesajili jumla ya visa 170,041 kutoka kwa sampuli 1,801,449.

Katika visa hivi vipya, 334 ni raia wa Kenya huku 10 wakiwa raia wa kigeni, 198 ni wa kiume na 146 ni wanawake.

Mgonjwa mwenye umri wa chini ana miezi 2 huku mwenye umri wa juu akiwa na miaka 93.

Kulingana na takwimu za wizara ya afya watu 30  wamepona virusi vya corona,3 walipona wakiwa nyumbani huku 27 wakipona wakiwa katika hospitali mbali mbali, na kufikisha idadi jumla ya 116,018 ya watu waliopona.

Hata hivyo habari za kuhuzunisha ni kwamba watu 16 wameaga dunia kutokana na maambukizi kufikisha 3,124 watu waliofariki kutokana na maambukizi ya virusi vya corona.

Jumla ya wagonjwa 1,188 wamelazwa katika vituo mbali mbali vya afya , huku 4,712 wakiuguzwa nyumbani.

Wagonjwa 107 wamo katika kitengo cha wagonjwa mahututi (ICU).

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved