logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Washukiwa katika shambulio la risasi dhidi ya Jenerali wa Uganda waonyeshwa kwenye CCTV

Picha za video za CCTV zinawaonesha watu wawili. Mmoja wao amevalia fulana ya blu yenye mistari.

image
na Radio Jambo

Habari02 June 2021 - 12:37

Muhtasari


  • Nitazidi kupigania maisha yangu, Jenerali Katumba azungumza baada ya shambulio

Polisi nchini Uganda wametoa picha za mtaani za CCTV za wanaume wawili wanaoaminiwa kuhusika na jaribio la kumuua Waziri wa uchukuzi nchini humo.

Gari la Jenerali Katumba Wamala lilinyunyiziwa risasi na watu wenye silaha waliokuwa kwenye pikipiki, na kumuua binti yake pamoja na dereva.

Inadhaniwa kuwa alikuwa akifuatwa na washambuliaji kwa mbali kabla ya shambulio la Jumanne.

Picha za video za CCTV zinawaonesha watu wawili. Mmoja wao amevalia fulana ya blu yenye mistari.

Moja ya pikipiki hizo iligeuza eneo ambalo sio mbali kutoka eneo la tukio la shambulio, kabla ya kutoweka ndani ya kituo cha petroli.

Hakuna hata sura ya mmoja wao inayoweza kutambulika.

Kikosi cha pamoja cha ujasusi cha polisi, na jeshi kinachunguza tukio hilo la ufyatuaji risasi.

Jeshi linasema linachunguza simu ambazo zinaonekana kuwa zilitumiwa kufanya mpango wa jaribio la mauaji.

Uganda imeshuhudia mashambulio kadhaa ya aina hiyo ya watu maarufu katika kipindi cha miaka michache iliyopita.

Huduma za ujasusi hazijaweza kutatua kisa chochote.

Kupitia kwenye ukrasa wake wa twitter jenerali huyo aliwashukuru wale wamekuwa wakimjulia hali na kutuma risala za rambi rambi kwa kumpoteza bintiye.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved