logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nimerudi! Msanii Bahati atangaza kutoa albamu mpya

Msanii huyo alisema kwamba anaenda kutoa albamu mpya na ya kupigiwa mfano na wengi.

image
na Radio Jambo

Habari04 June 2021 - 12:05

Muhtasari


  • Msanii arejea mitandaoni na habari njema
  • Kulingana na msanii huyo, wasanii  wa humu nchini wanapaswa kuketi kitako na kalamu na kitabu na kunakili yale anaenda kufanya

Siku chache zilizopita msanii Kevin Bahati kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram alitangaza kuchukua mapumziko kutoka kwenye mitandao ya kijamii.

Haya basi habari njema kwa mashabiki ni kwamba amerejea, na hajarejea tu bali amerudi na habari njema.

Kulingana na msanii huyo, wasanii  wa humu nchini wanapaswa kuketi kitako na kalamu na kitabu na kunakili yale anaenda kufanya.

Msanii huyo alisema kwamba anaenda kutoa albamu mpya na ya kupigiwa mfano na wengi.

"NIMERUDI!!! nilichukua Mapumziko ya Siku chache Kuruhusu Msanii yeyote Anayetaka Kutoa Wimbo, EP au Albamu ya Kufanya Hivyo! 

Kwa hivyo ikiwa bado haujafanya hivyo Wakati umekwisha! Pumzika ... Siku 90 Zifuatazo Zitakuwa Zangu!

Ndio wakati wa albamu yangu ya kuweka miaka yangu7 kwenye tasnia ya muziki !!! Sijui Kuweka haya au kusema ili bado niwe mnyanyekevu Waambie Wanamuziki wenzako wapumzike tu, Kaa chini Chukua Kitabu cha Kumbuka niko karibu kuwafundisha Jinsi ya kutengeneza albamu yenye ina nyimbo za kuvuma !!! Ndio nimesema .... LEO USIKU SAA 7 JIONI NAFICHUA JINA LA albamu 💽," Alisema Bahati.

Haya basi tunangoja, na mashabiki wanangoja kwa hamu kusikia jina la albamu hiyo na jinsi itakavyo kuwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved