logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wasiwasi baada ya mwanamuziki kudai kuwa angefariki Ijumaa usiku

Wakenya wengi ikiwemo wasanii wenzake wamefanya juhudi za kuwasiliana na  Magix Enga  ila hakuna aliyetangaza kufanikiwa kumfikia

image
na Radio Jambo

Habari05 June 2021 - 08:14

Muhtasari


•King Kaka na Kristoff ni baadhi ya wasanii ambao wameeleza kuwa juhudi za kumfikia Magix Enga hazijafua dafu.

Magix Enga

Hali ya wasiwasi imetanda katika mtandao wa Instagram baada ya mwanamuziki na mtengezaji wa nyimbo Magix Enga kuchapisha ujumbe kuwa angefariki usiku wa kuamkia Jumamosi.

Mwanamuziki huyo wa nyimbo aina ya gengetone alichapisha ujumbe "I'm gonna die tonight"(nitafariki usiku wa leo) mida ya saa nne unusu usiku.

Aliendelea kusema kuwa angepenza kila mtu.

'"I'm going to miss everyone"(Nitawapeza nyote)"

Haijabainika wazi kilichomfanya Enga kuchapisha ujumbe huo ambao umeshtua Wakenya wengi huku wengine wakibashiri kuwa huenda ni huzuni.

Wakenya wengi ikiwemo wasanii wenzake wamefanya juhudi za kuwasiliana na mwanamuziki huyo ila hakuna aliyetangaza kufanikiwa kumfikia.

Jumbe za King Kaka na Kristoff

King Kaka na Kristoff ni baadhi ya wasanii ambao wameeleza kuwa juhudi za kumfikia Magix Enga hazijafua dafu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved