logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mhubiri mashuhuri TB Joshua aaga dunia

TB Joshua ameaga akiwa na umri wa miaka 57, siku sita tu kabla ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa.

image
na Radio Jambo

Habari06 June 2021 - 08:28
TB Joshua

Mwinjilisti maarufu wa Nigeria TB Joshua ameaga dunia.

TB Joshua ameaga akiwa na umri wa miaka 57, siku sita tu kabla ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa.

Kifo chake kilithibitishwa na kanisa lake la Sinagogi la Mataifa Yote ((The Synagogue Church of All Nations) Jumapili asubuhi.  

Kupitia mitandao yao ya kijami, kanisa hilo lilitangaza;

"Mungu amemchukua mtumishi wake Nabii TB Joshua kwenda naye nyumbani - kama inavyopaswa kuwa kwa mapenzi ya mungu. Nyakati zake za mwisho hapa duniani zilitumika katika kumtumikia Mungu. Hiki ndicho alichozaliwa, kuishi na kufa." Kanisa lake lilitangaza kifo chake.

Alizaliwa mnamo Juni 12, 1963, huko Arigidi.

Mipango ilikuwa ikiendelea ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa.

Habari za kifo chake zilienea katika mitandao ya kijamii mapema asubuhi ya Jumapili huku wafuasi na wananchi wa Nigeria wakimuomboleza nabii huyo.

Kulingana na taarifa kadhaa, nabii huyo aliugua siku chache zilizopita.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved