logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Visa vya wanaume kujitoa uhai vimezidi - Utafiti

Mwanasaikolojia Silas Kirinya anasema ingawaje wanawake wengi zaidi hujaribu kujitoa uhai, wanaume wengi zaidi hufanikiwa kwani si rahisi kwao kufunguka, kwa kuogopa unyanyapaa.

image
na Radio Jambo

Habari06 June 2021 - 05:50
stress (1)

Upatikanaji wa rahisi wa siaha, na shinikizo la matarajio ya jamii kwamba mwanamume anafaa kuwa jasiri au ataonekana kuwa mdhaifu, huenda ikawa baadhi ya sababu zinazowapelekea wanaume wengi kujitoa uhai, kuliko wanawake.

Mwanasaikolojia Silas Kirinya anasema ingawaje wanawake wengi zaidi hujaribu kujitoa uhai, wanaume wengi zaidi hufanikiwa kwani si rahisi kwao kufunguka, kwa kuogopa unyanyapaa.

tukisalia katika maswala ya wanaume, ni wanaume wachache walio na maradhi ya akili hutafuta usaidizi, kutokana na aibu inayohusishwa na hali hii.

Mwanasaikolojia Silas Kirinya anasema wanaume wanapaswa kuelewa kuwa maradhi ya akii yanaweza kumuathiri mtu yeyote, kwa hivyo kutafuta usaidizi sio ishara ya kuwa mdhaifu.

Kwingineko, watu waliojawa na ghadhabu walimpiga hadi kumuua na kumzika mwanamume mmoja mwenye umri wa miaka 28 anayetuhumiwa kumuua mamake Jumatano usiku, huko Kivingoti, Ndia kaunti ya Kirinyaga.

Mwanamume huyo anasemekana kutoroka na kisha kuregea, akiwa na nia ya kumuua nduguye. Wakaazi wanasema sasa wamepata afueni kwani walikuwa wanaishi kwa hofu ya kushambuliwa.

Hayo yakijiri, mlalamishi mmoja ameiandikia mahakama ya rufaa, akimtaka rais Uhuru Kenyatta kuwajibishwa kibinafsi kuregesha fedha zilizotumika kuipigia debe BBI, kwa hazina ya kitaifa. Kupitia kwa wakili Morara Omoke, mlamishi huyo pia anaitaka mahakama kumshurutisha rais kulivunjilia mbali bunge, kulingana na ushauri wa aliyekuwa jaji mkuu David Maraga, kwa kukosa kutimiza sheria ya kijinsia ya thuluthi mbili.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved