logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanajeshi Mmarekani apigwa faini ya 70,000 kwa kumshambulia polisi Gigiri

Inadaiwa kuwa Stanley alimshika konstabo Kamau shingoni, akamtoa barakoa kisha akamgonga kwenye jicho lake la kushoto  kabla ya konstabo Henry Kibet ambaye walikuwa zamu naye kuja kumsaidia.

image
na Radio Jambo

Habari20 June 2021 - 06:20

Muhtasari


•Zarnoch Stanley alikubali shtaka alilokabiliwa nalo mbele ya hakimu mkuu  katika mahakama ya Kibera, Charles Mwaniki  na kuhukumiwa kifungo cha mwaka mmoja iwapo atakaidi faini aliyotozwa.

•Alipokuwa anahukumiwa, aliagiza mahakama kumuonea huruma huku akidai kuwa alikuwa anatumia dawa kwani alikuwa anaugua.

Zarnoch Stanley katika mahakama ya Kibera

Mwanaume mmoja ambaye  alikuwa mwanajeshi wa anga Marekani amepigwa faini ya Sh70000 kwa kushambulia afisa wa polisi.

Zarnoch Stanley alikubali shtaka alilokabiliwa nalo mbele ya hakimu mkuu  katika mahakama ya Kibera, Charles Mwaniki  na kuhukumiwa kifungo cha mwaka mmoja iwapo atakaidi faini aliyotozwa.

Stanley alishtakiwa kumshambulia konstabo Kamau Muthoni katika kiingilio cha ofisi za shirika la uhamisho zilizo Gigiri na kumpiga mangumi kwenye uso na mkono kisha kumkanyanga mguu mnamo  tarehe 2 mwezi huu.

Alikuwa ameandamana na mwanamke Mwafrika anayeaminika kuwa mpenzi wake na ambaye alikuwa na miadi katika ofisi za shirika uhamiaji wakati tukio hilo lilitokea. 

Mmarekani huyo alizuiliwa kupita baada ya mwenzake  kuingia kulingana na sheria za shirika lile na akaagizwa kumsubiri nje ya lango.

Kufuatia hayo, mwanajeshi huyo mstaafu alianza kumtishia Kamau huku akimtupia maneno machafu.

Inadaiwa kuwa Stanley alimshika konstabo Kamau shingoni, akamtoa barakoa kisha akamgonga kwenye jicho lake la kushoto  kabla ya konstabo Henry Kibet ambaye walikuwa zamu naye kuja kumsaidia.

Alikamatwa na kuzuiliwa katika kituo cha polisi kufuatia kitendo hicho.

Alipokuwa anahukumiwa, aliagiza mahakama kumuonea huruma huku akidai kuwa alikuwa anatumia dawa kwani alikuwa anaugua.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved