logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Martha Koome ahamisha majaji katika mahakama ya kukata rufaa; Apatia wapya vituo vya kuhudumu

Majaji hao ishirini wanafaa kuripoti katika vituo vyao mnamo Julai 1.

image
na Radio Jambo

Habari22 June 2021 - 05:33

Muhtasari


•Akitangaza mabadiliko hayo kupitia ujumbe kwa wanahabari siku ya Jumanne, Koome alisema kuwa yote yalifanyika baada ya mashauriano na rais wa mahakama ya kukata rufaa, Jaji Daniel Musinga.

•Mahakama ya Mombasa na Kisumu ambazo zilikuwa zimefungwa mwaka wa 2019 kufuatia upungufu wa majaji zitafunguliwa kabisa kwani kuna majaji ambao watakuwa wanahudumu pale.

Jaji Martha Koome

Jaji mkuu Martha Koome ametangaza kuhamishwa kwa majaji wa mahakama ya kukata rufaa huku walioteuliwa hivi majuzi wakipewa mahakama za kufanyia kazi.

Akitangaza mabadiliko hayo kupitia ujumbe kwa wanahabari siku ya Jumanne, Koome alisema kuwa yote yalifanyika baada ya mashauriano na rais wa mahakama ya kukata rufaa, Jaji Daniel Musinga.

"Uhamisho huu umefanyika kulingana na sera ya uhamisho ya mahakama ya kukata rufaa ambayo inasema muda ambao jaji anafaa kuhudumu katika kituo kimoja kati ya mambo mengine" Ujumbe huo ulisoma.

Jumla ya majaji wa mahakama ya kukata rufaa ilifikia 20 baada ya majaji saba  wapya kuidhinishwa na rais Uhuru Kenyatta na kuapishwa mnamo Juni 4 .

Mahakama ya Mombasa na Kisumu ambazo zilikuwa zimefungwa mwaka wa 2019 kufuatia upungufu wa majaji zitafunguliwa kabisa kwani kuna majaji ambao watakuwa wanahudumu pale.

Jaji Daniel Musinga atakuwa ambaye aliapishwa kuwa rais wa mahakama hiyo atahudumu katika koti ya Nairobi

Wengine ambao watahudumu katika koti mbalimbali jijini Nairobi ni pamoja na jaji Roselyn Nambuye, Wanjiru Karanja, Hannah Okwengu,Mohammed Warsame, Asike Makhandia, Kathurima M'Inoti, Agnes Murgor, Fatuma Sichale, Jamila Mohammed, Sankale Ole Kantai, Msaga Mbogholi, Hellen Omondi na jaji Imaana Laibuta.

Jaji Patrick O. Kiage atahudumu Kisumu pamoja na jaji Mumbi Ngugi na Francis Tuiyott huku jaji Pauline Nyamweya na Jesie Lesiit wakihudumu Mombasa.

Majaji hao ishirini wanafaa kuripoti katika vituo vyao mnamo Julai 1.

 

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved