logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jinsia ya mtoto wa Vera Sidika hatimaye yafichuliwa

Brown Mauzo lazima afurahi sana juu ya habari ya jinsia ya mwanawe kwani alikuwa na matumaini.

image
na Radio Jambo

Habari11 July 2021 - 04:53

Muhtasari


  • Jinsia ya mtoto wa Vera Sidika hatimaye yafichuliwa
  • Mjasiriamali  na mwanasosholaiti Vera Sidika  mwenye ujauzito anastahili kujifungua baada ya miezi mitatu
  • Vera mpenzi wake Brown Mauzo wanatarajia mtoto wao wa kwanza au kifungua mimba wao
Vera Sidika akifichua mimba

Mjasiriamali  na mwanasosholaiti Vera Sidika  mwenye ujauzito anastahili kujifungua baada ya miezi mitatu.

Vera mpenzi wake Brown Mauzo wanatarajia mtoto wao wa kwanza au kifungua mimba wao.

Vera, ambaye anafurahi sana kukaribisha kifurushi chake cha furaha, alifanya sherehe nzuri ya kufichua jinsia Jumamosi, Julai 10, jijini Nairobi.

Na baada yautni mwingi kutoka kwa Vera, mwishowe ilifichuliwakuwa anatarajia mtoto msichana.

Hii inatimiza tu matakwa ya mumewe, Brown Mauzo ambaye alikuwa na matumaini kuwa watapata mtoto wa kike.

Brown Mauzo lazima afurahi sana juu ya habari ya jinsia ya mwanawe kwani alikuwa na matumaini.

Kabla ya siku ya sherehe, Vera Sidika hakuweza kuficha wasiwasi wake kwani alitamani kujua jinsia ya mtoto

Kulingana na mchekeshaji Eric Omondi, endapo wanandoa watapata kifunua mimba msichana walikuwa na mapenzi tele, ilhali wakimpata mvulana kweli walifanya tendo la ndoa, alimtania Vera Sidika.

Awali kwenye ukurasa wake wa instagram aliweka wazi kwamba alibeba ujauzito wake siku ya wapendanao mwaka huu.

Kutoka kwetu wanajambo tunamtakia mwanasosholait huyo kila la heri.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved