logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Unyama!Masten Wanjala,20,Akiri Kuteka Nyara, Kunyonga Watoto Wawili Kabete

Katika ufichuzi mpya, Wanjala amekiri kuwateka nyara na kuwanyonga watoto hao.

image
na Radio Jambo

Habari14 July 2021 - 13:21

Muhtasari


  • Masten Wanjala,20,Akiri Kuteka Nyara, Kunyonga Watoto Wawili Kabete

Masten Milimu Wanjala, kijana wa miaka 20 amekiri kuteka nyara, kunyonga watoto wawili  huko Kabete.

Wanjala alikamatwa hapo awali na maafisa wa upelelezi kutoka kwa DCI katika eneo la Shauri Moyo kwa tuhuma za kuua watoto wawili wenye umri wa miaka 13 na 12 kwa tarehe tofauti.

Watoto hao, waliotambuliwa kama Charles Opindo Bala, 13 aliyepotea mnamo Juni 30, 2021, na Mutuku Musyoka, 12 ambaye alipotea Julai 8, walipatikana kwenye kichaka huko Kabete, Kaunti ya Kiambu.

Katika ufichuzi mpya, Wanjala amekiri kuwateka nyara na kuwanyonga watoto hao.

Aliongoza maafisa wa upelelezi mahali ambapo alifanya vitendo vya kinyama na kuitoa miili hiyo huko Kabete.

Kabla ya hapo, Wanjala alikuwa amewasiliana na mama wa Musyoki, Felista Wayua, akidai fidia ya Shilingi 50,000 ili mtoto wake awe huru.

Baba ya Opindo Tony Opindo, ambaye mtoto wake hakuwahi kurudi nyumbani kutoka Shule ya Msingi Sagaret huko Majengo, aliulizwa kutuma Shilingi 30,000 kununua uhuru wa mtoto wake.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved