logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Hii nyumba sio ya kuuzwa!' Omosh aahidi kutouza nyumba mpya aliyojengewa

Kumekuwa na hofu miongoni mwa Wakenya kuwa huenda mwigazaji huyo ambaye amekuwa mhasiriwa wa uraibu wa pombe kwa muda akauza nyumba hiyo ili aweze kukata kiu.

image
na Radio Jambo

Habari14 July 2021 - 20:09

Muhtasari


•Omosh alikabidhiwa nyumba ambayo alijengewa na wadhamini siku ya Jumatano kwenye hafla iliyohudhuriwa na baadhi ya wasanii mashuhuri kama vile Jalango, Fred Omondi, DJ Shiti kati ya wengine.

•Mtangazaji Jalang'o alimkabidhi bango ambalo lilikuwa limeandikwa 'Mali hii si ya kuuzwa' na akampa ushauri kuwa asishawishike kuuza nyumba ile.

Hatimaye aliyekuwa mwigizaji wa Tahidi  High Joseph Kinuthia almaarufu kama Omosh anajivunia kuwa mmiliki rasmi wa nyumba.

Omosh alikabidhiwa nyumba ambayo alijengewa na wadhamini siku ya Jumatano kwenye hafla iliyohudhuriwa na baadhi ya wasanii mashuhuri kama vile Jalango, Fred Omondi, DJ Shiti kati ya wengine.

Kumekuwa na hofu miongoni mwa Wakenya kuwa huenda mwigazaji huyo ambaye amekuwa mhasiriwa wa uraibu wa pombe kwa muda akauza nyumba hiyo ili aweze kukata kiu.

Hata hivyo, Omosh aliahidi kuwa hatauza nyumba yake mpya na akatangaza hadharani kuwa nyumba ile si ya kuuzwa.

"Kwetu kuna mila na desturi kuwa huwezi patiwa zawadi ukapatia mtu mwingine kama zawadi ama ukaiuza. Hii ni zawadi na haiwezi uzwa" Omosh alisema.

Mtangazaji Jalang'o alimkabidhi bango ambalo lilikuwa limeandikwa 'Mali hii si ya kuuzwa' na akampa ushauri kuwa asipatwe na tamaa ya  kuuza nyumba ile.

Jalang'o alimwambia Jalang'o aarifu wale ambao walikuwa wakimezea mate nyumba hiyo kuwa si ya kuuzwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved