logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Koplo Caroline Kangogo ajitoa uhai kwa kujipiga risasi kichwani

Inadaiwa kuwa Kangogo amejiuwa kwa kujipiga risasi akiwa nyumbani kwa wazazi wake maeneo ya Elgeyo Marakwet.

image
na Radio Jambo

Habari16 July 2021 - 06:54

Muhtasari


•Inadaiwa kuwa Kangogo amejiuwa kwa kujipiga risasi kichwani akiwa nyumbani kwa wazazi wake maeneo ya Elgeyo Marakwet.

Mshukiwa katika mauaji ya watu wawili,  koplo Caroline Kangogo amejitia kitanzi.

Inadaiwa kuwa Kangogo amejiuwa kwa kujipiga risasi akiwa nyumbani kwa wazazi wake maeneo ya Elgeyo Marakwet.

Akithibitisha tukio hilo, kamanda wa polisi maeneo ya Keiyo, Tom Makori amesema kuwa Kangogo alijipiga risasi  kwa kutumia bastola akiwa ndani ya bafu.

Inadaiwa kuwa huenda Kangogo alifika kwao jioni ya siku ya Alhamisi.

Polisi wamekuwa wakimuwinda Kangogo baada yake kutekeleza mauaji ya kinyama dhidi ya wanaume wawili maeneo ya Nakuru na Juja.

Hapo awali, wazazi wa Kangogo walikuwa wamemuomba mwanadada huyo kujisalimisha.

Maafisa wa kukabiliana na uhalifu wametumwa katika eneo hilo.

Hata hivyo, utata umeibuka kuhusu kifo hicho huku baadhi ya watu wakidai kuwa huenda Kangogo hakujitoa uhai mwenyewe.

 

Mengi yatafuata.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved