logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Vurugu Kiambaa baada ya Jubilee kudai kuwepo kwa ulaghai katika uhesabu wa kura

Kariri Njama akiungwa mkono na wafuasi wake wamekabiliana na maafisa wa usalama wakiagiza kuhesabiwa tena kwa kura za vituo vitatu.

image
na Radio Jambo

Habari16 July 2021 - 02:49

Muhtasari


•Kufikia sasa Njuguna wa UDA anaongoza akiwa na kura 21,606 huku akifuatwa kwa karibu na Kariri Njama wa Jubilee akiwa na kura 21, 151.

Huku ikiwa imebaki kutangazwa kwa matokeo ya kituo cha kupigia kura kimoja tu ili mshindi wa kinyang'anyiro cha Kiambaa ajulikane, vurugu zimeshuhudiwa katika kituo cha kuhesabia kura cha Karuri baada ya mgombea kiti na tikiti ya Jubilee kudai kuwepo kwa wizi wa kura.

Kariri Njama akiungwa mkono na wafuasi wake wamekabiliana na maafisa wa usalama wakiagiza kuhesabiwa tena kwa kura za vituo vitatu.

Mwanasiasa huyo na wafuasi wake hawakuridhishwa na matokeo ambayo yalitangazwa kutoka vituo vya Cianda, Gachie na Muchatha. Walidai kuwa matokeo yalikuwa yamebadilishwa kwa mapendeleo mgombea kiti na tikiti ya UDA John Njuguna.

Kufikia sasa Njuguna wa UDA anaongoza akiwa na kura 21,606 huku akifuatwa kwa karibu na Kariri Njama wa Jubilee akiwa na kura 21, 151.

Matokeo rasmi yanatarajiwa kutangazwa baada ya kujumuishwa kwa matokeo ya kituo cha mwisho kilichobaki.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved